Bwana Yesu asifiwe!
Wakati kampeni zinaendelea na tarehe ya Uchaguzi inazidi kukaribia unakumbushwa kuendelea kuuombea Uchaguzi Mkuu unaofanyika siku ya Jumapili ya Tarehe 25/10/2015.
Yako mambo mengi ambayo yanahitaji msaada wa Mungu. Wakati unaombea uchaguzi huu unaweza pia kukumbuka kuombea hafuatayo:
– Mungu awape afya njema wagombea wote hadi uchaguzi ukamilike.
– Mungu aepushe ajali za misafara ya kampeni.
– Hila zozote mbaya kinyume na uchaguzi zikadhihirike na kuharibiwa
-Hekima, maarifa na Uzalendo vikatawale kampeni ili kuepusha vurugu na mifarakano isiyo ya lazima!
Mungu akubariki unapoendelea kuombea Uchaguzi huu.
Filed under: KUTOKA S.G
